Kanuni ya Imani
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, mwumba mbingu na dunia. 
Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu, 
akazaliwa na Bikira Maria, 
akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, 
akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; 
siku ya tatu akafufuka katika wafu;
 akapaa mbinguni; amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi;
 toka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu. 
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,
 Kanisa takatifu katoliki, 
ushirika wa Watakatifu,
 maondoleo ya dhambi,
 ufufuko wa miili, uzima wa milele.
 Amina.
                                
                                0 Imependwa
                                0 Maoni 
                            
                            
                        
Maoni
Ingia utoe maoni