Sala ya Usiku
Sasa siku imekwisha,
Kwako Mungu napandisha,
moyo wangu kwa shukrani,
nipumzike kwa amani,
Mema mengi umenipa,
ninashindwa kukulipa,
Baba mwema ondolea,
yote niliyokosea.
Yesu mpenzi unijie,
ombi langu usikie,
unifiche mtoto wako,
ndani ya jeraha zako,
Ewe Mama unipe neema,
raha na usiku mwema,
Roho mlizi ukakeshe,
pepo wasinikoseshe
Naiweka roho yangu,
mikononi mwa Baba yangu,
bila hofu napumzika,
mwisho kwake nitafika.
Amina
                                
                                0 Imependwa
                                0 Maoni 
                            
                            
                        
Maoni
Ingia utoe maoni