Ijumaa. 07 Agosti. 2026

Sala

Sala ya Usiku

Sasa siku imekwisha,
Kwako Mungu napandisha,
moyo wangu kwa shukrani,
nipumzike kwa amani,

Mema mengi umenipa,
ninashindwa kukulipa,
Baba mwema ondolea,
yote niliyokosea.

Yesu mpenzi unijie,
ombi langu usikie,
unifiche mtoto wako,
ndani ya jeraha zako,

Ewe Mama unipe neema,
raha na usiku mwema,
Roho mlizi ukakeshe,
pepo wasinikoseshe

Naiweka roho yangu,
mikononi mwa Baba yangu,
bila hofu napumzika,
mwisho kwake nitafika.

Amina

Maoni

Elia Stanley Mlay

Ee Mungu naomba usiku huu ninapoenda kulala ukanikinge na pepo wachafu,majinamizi,wachawi,vibwengo ,nilale salama pamoja na watoto wangu sita AMEN

Andrew Timotheo

Ee MUNGU mwingi wa rehema na baraka uturinde usiku huu mimi na familia yangu utupe usingizi mnono mikononi mwako vichwa vyetu twajilaza wewe uu mkuu leo hata milele Amina

Joseph Marekani

Ee mungu nibaliki tunapo enda kulala maraika mlinzi awe pamoja nasi na tuamke na fulaha na upendo amina

Marekani Nestory

Mungu wangu wabaliki watu ote wanao fuatilia mkatoliki leo walale salama na waamke wenyenguvu na afya tele amina

GASPER MKELEMI

amina

DAVID ELIA

Hacha mungu akubariki sisi zote katika usiku ya leo

Leokadia Pius

Hii sala ni nzuri sana ndugu wakristo wenzangu unapaswa kumshuru mungu kwa yote aliyokutendea toka asubuhi mpak jion

Donata Musa

Mm kila ck jion namshukulu mungu mwenyezi

Ngelela. Ngusa.

Mungu ni wetu sote,hivyo tujitahidi kuwashauri wasiomjua mungu wamjue kwani ndio msaada na kimbilio letu wanadamu.Amina.

fulugenzi mapunda

asande mungu

fulugenzi mapunda

Sasande mungu wangu

Donata Musa

Tusal kila ck jaman wapenz wa mungu sala za asubuhi na za jion

Kamgisha Elipidius

Mungu wangu huturinde usiku huu wa leo ilinde familly yangu waponye wagonjwa waliopo majumbani na huko hospitari bwana niongoze kwenye kazi zangu ubavuni mwako nifiche adui zangu wasinipate mungu shusha maraika wako watuzingire mahari hapa bwana nashukru haya machache uliyonipatia naomba hayo kwa jina la mwanao kipenzi yesu kristo. amen

Ingia utoe maoni