Sala ya Usiku
Sasa siku imekwisha,
Kwako Mungu napandisha,
moyo wangu kwa shukrani,
nipumzike kwa amani,
Mema mengi umenipa,
ninashindwa kukulipa,
Baba mwema ondolea,
yote niliyokosea.
Yesu mpenzi unijie,
ombi langu usikie,
unifiche mtoto wako,
ndani ya jeraha zako,
Ewe Mama unipe neema,
raha na usiku mwema,
Roho mlizi ukakeshe,
pepo wasinikoseshe
Naiweka roho yangu,
mikononi mwa Baba yangu,
bila hofu napumzika,
mwisho kwake nitafika.
Amina
1 Imependwa
10 Maoni

Maoni
Elia Stanley Mlay
Ee Mungu naomba usiku huu ninapoenda kulala ukanikinge na pepo wachafu,majinamizi,wachawi,vibwengo ,nilale salama pamoja na watoto wangu sita AMENAndrew Timotheo
Ee MUNGU mwingi wa rehema na baraka uturinde usiku huu mimi na familia yangu utupe usingizi mnono mikononi mwako vichwa vyetu twajilaza wewe uu mkuu leo hata milele AminaJoseph Marekani
Ee mungu nibaliki tunapo enda kulala maraika mlinzi awe pamoja nasi na tuamke na fulaha na upendo aminaMarekani Nestory
Mungu wangu wabaliki watu ote wanao fuatilia mkatoliki leo walale salama na waamke wenyenguvu na afya tele aminaGASPER MKELEMI
aminaDAVID ELIA
Hacha mungu akubariki sisi zote katika usiku ya leoLeokadia Pius
Hii sala ni nzuri sana ndugu wakristo wenzangu unapaswa kumshuru mungu kwa yote aliyokutendea toka asubuhi mpak jionNgelela. Ngusa.
Mungu ni wetu sote,hivyo tujitahidi kuwashauri wasiomjua mungu wamjue kwani ndio msaada na kimbilio letu wanadamu.Amina.fulugenzi mapunda
asande mungufulugenzi mapunda
Sasande mungu wanguIngia utoe maoni